25 Absalomu alimweka Amasa+ kuwa msimamizi wa jeshi badala ya Yoabu;+ Amasa alikuwa mwana wa mwanamume Mwisraeli aliyeitwa Ithra, aliyelala na Abigaili,+ binti ya Nahashi, dada ya Seruya, mama ya Yoabu.
10 Amasa hakuchukua tahadhari kuhusiana na upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, basi Yoabu akamchoma tumboni kwa upanga huo,+ na matumbo yake yakamwagika ardhini. Hakuhitaji kumchoma tena; alikufa alipochomwa mara moja. Kisha Yoabu na ndugu yake Abishai wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.