Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 16:30, 31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Ahabu mwana wa Omri alikuwa mwovu sana machoni pa Yehova kuliko wote waliomtangulia.+ 31 Na kana kwamba lilikuwa jambo dogo kwake kutembea katika dhambi za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, hata alimwoa Yezebeli+ binti ya Ethbaali, mfalme wa Wasidoni,+ akaanza kumwabudu Baali+ na kumwinamia.

  • 2 Wafalme 3:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Yehoramu+ mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli kule Samaria katika mwaka wa 18 wa utawala wa Mfalme Yehoshafati wa Yuda, naye alitawala kwa miaka 12.

  • 2 Wafalme 3:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Hata hivyo, alishikamana na dhambi ambazo Yeroboamu mwana wa Nebati alikuwa amesababisha Waisraeli watende.+ Hakuziacha.

  • 2 Wafalme 10:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Lakini Yehu hakuwa mwangalifu kutembea katika Sheria ya Yehova Mungu wa Israeli kwa moyo wake wote.+ Hakugeuka na kuacha dhambi ambazo Yeroboamu alisababisha Waisraeli kutenda.+

  • 2 Wafalme 13:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Katika mwaka wa 23 wa utawala wa Yehoashi+ mwana wa Ahazia+ mfalme wa Yuda, Yehoahazi mwana wa Yehu+ akawa mfalme wa Israeli huko Samaria, naye alitawala kwa miaka 17. 2 Aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, na kuendelea kutenda dhambi ya Yeroboamu mwana wa Nebati aliyosababisha Waisraeli kutenda.+ Hakugeuka na kuiacha.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki