-
1 Wafalme 10:16, 17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Mfalme Sulemani alitengeneza ngao kubwa 200 za dhahabu iliyochanganywa na madini mengine+ (kwa kila ngao alitumia shekeli 600* za dhahabu)+ 17 na ngao ndogo* 300 za dhahabu iliyochanganywa na madini mengine (kwa kila ngao ndogo alitumia mina tatu* za dhahabu). Kisha mfalme akaziweka katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni.+
-
-
2 Mambo ya Nyakati 12:9-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Basi Mfalme Shishaki wa Misri akashambulia Yerusalemu. Akachukua hazina za nyumba ya Yehova+ na hazina za nyumba ya* mfalme. Alichukua kila kitu, kutia ndani ngao za dhahabu ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza.+ 10 Basi Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba zichukue mahali pa ngao hizo, akaziweka chini ya ulinzi wa mkuu wa walinzi,* aliyelinda mlango wa nyumba ya mfalme. 11 Wakati wowote ambapo mfalme alikuja katika nyumba ya Yehova, walinzi waliingia ndani na kuzichukua, kisha walizirudisha katika chumba cha walinzi.
-