Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 13:1-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 “Ikiwa nabii au mtu anayebashiri kupitia ndoto atatokea miongoni mwenu na kuwapa ishara au dalili ya ajabu, 2 kisha ishara au dalili hiyo aliyowaambia itimie wakati anaposema, ‘Acheni tuifuate miungu mingine, miungu msiyoijua, na acheni tuiabudu,’ 3 hampaswi kusikiliza maneno ya nabii huyo au mwotaji huyo wa ndoto,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu anawajaribu+ ili ajue ikiwa mnampenda Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+ 4 Mnapaswa kumfuata Yehova Mungu wenu, mnapaswa kumwogopa yeye, mnapaswa kushika amri zake, mnapaswa kuisikiliza sauti yake; yeye ndiye mnayepaswa kumtumikia, nanyi mnapaswa kushikamana naye kabisa.+ 5 Lakini nabii huyo au mwotaji huyo wa ndoto anapaswa kuuawa,+ kwa sababu aliwachochea mmwasi Yehova Mungu wenu—aliyewatoa nchini Misri na kuwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa—ili mtoke katika njia ambayo Yehova Mungu wenu amewaamuru mtembee. Nanyi lazima mwondoe kilicho kiovu kutoka miongoni mwenu.+

  • Kumbukumbu la Torati 18:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 “‘Ikiwa nabii yeyote atasema kwa kimbelembele katika jina langu neno ambalo sikumwamuru aseme au kusema katika jina la miungu mingine, nabii huyo lazima afe.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki