Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 13:1-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 “Ikiwa nabii au mtu anayebashiri kupitia ndoto atatokea miongoni mwenu na kuwapa ishara au dalili ya ajabu, 2 kisha ishara au dalili hiyo aliyowaambia itimie wakati anaposema, ‘Acheni tuifuate miungu mingine, miungu msiyoijua, na acheni tuiabudu,’ 3 hampaswi kusikiliza maneno ya nabii huyo au mwotaji huyo wa ndoto,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu anawajaribu+ ili ajue ikiwa mnampenda Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+ 4 Mnapaswa kumfuata Yehova Mungu wenu, mnapaswa kumwogopa yeye, mnapaswa kushika amri zake, mnapaswa kuisikiliza sauti yake; yeye ndiye mnayepaswa kumtumikia, nanyi mnapaswa kushikamana naye kabisa.+ 5 Lakini nabii huyo au mwotaji huyo wa ndoto anapaswa kuuawa,+ kwa sababu aliwachochea mmwasi Yehova Mungu wenu—aliyewatoa nchini Misri na kuwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa—ili mtoke katika njia ambayo Yehova Mungu wenu amewaamuru mtembee. Nanyi lazima mwondoe kilicho kiovu kutoka miongoni mwenu.+

  • Yeremia 28:11-17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Kisha Hanania akasema mbele ya watu wote: “Yehova anasema hivi: ‘Hivyo ndivyo nitakavyoivunja nira ya Mfalme Nebukadneza wa Babiloni kutoka shingoni mwa mataifa yote katika muda wa miaka miwili.’”+ Kisha nabii Yeremia akaenda zake.

      12 Baada ya nabii Hanania kuivunja ile nira kutoka shingoni mwa nabii Yeremia, ujumbe huu wa Yehova ukamjia Yeremia: 13 “Nenda umwambie Hanania, ‘Yehova anasema hivi: “Umevunja nira za mbao,+ lakini badala yake utatengeneza nira za chuma.” 14 Kwa maana Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Nitaweka nira ya chuma juu ya shingo ya mataifa haya yote, ili yamtumikie Mfalme Nebukadneza wa Babiloni, nayo lazima yamtumikie.+ Nitampa hata wanyama wa mwituni.”’”+

      15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania:+ “Tafadhali, sikiliza, ewe Hanania! Yehova hakukutuma wewe, bali umewafanya watu hawa wautumaini uwongo.+ 16 Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘Tazama! Ninakuondoa katika uso wa nchi. Utakufa mwaka huu, kwa maana umewachochea watu wamwasi Yehova.’”+

      17 Basi nabii Hanania akafa mwaka huo, katika mwezi wa saba.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki