-
2 Wafalme 9:25, 26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Kisha akamwambia Bidkari kamanda wake msaidizi: “Mwinue na umtupe katika shamba la Nabothi, Myezreeli.+ Kumbuka kwamba mimi na wewe tulipokuwa tukiendesha magari ya farasi* tukimfuata Ahabu baba yake, Yehova mwenyewe alitangaza hivi dhidi yake:+ 26 ‘“Kwa hakika kama nilivyoona damu ya Nabothi+ na damu ya wanawe jana,” asema Yehova, “nitakulipa+ wewe katika shamba hilihili,” asema Yehova.’ Basi sasa mwinue na umtupe katika shamba hili, kulingana na neno la Yehova.”+
-