-
2 Mambo ya Nyakati 18:33, 34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 Lakini mtu fulani alivuta upinde wake bila kukusudia* na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya sehemu ambazo koti lake la vita linaungana. Basi mfalme akamwambia mtu aliyeendesha gari lake: “Geuka uniondoe vitani,* kwa sababu nimejeruhiwa vibaya.”+ 34 Vita vikapamba moto siku hiyo yote, nao wakalazimika kumsimamisha mfalme ndani ya gari, akiwaelekea Wasiria mpaka jioni; akafa jua lilipokuwa likitua.+
-