6 Tena Yehova akamwambia: “Tafadhali, utie mkono wako ndani ya mkunjo wa juu wa vazi lako.” Basi akautia mkono wake ndani ya mkunjo wa vazi lake. Alipoutoa, tazama, mkono wake ulikuwa umepigwa na ukoma, ukawa mweupe kama theluji!+
10 Lile wingu likaondoka juu ya hema, na tazama! Miriamu alikuwa amepigwa kwa ukoma mweupe kama theluji.+ Kisha Haruni akageuka na kumtazama Miriamu, akaona kwamba alikuwa amepigwa kwa ukoma.+