-
2 Wafalme 4:32-35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
32 Elisha alipoingia katika nyumba hiyo, mvulana huyo alikuwa amelala kwenye kitanda chake akiwa mfu.+ 33 Aliingia ndani, akajifungia humo pamoja na mvulana huyo na kuanza kusali kwa Yehova.+ 34 Kisha akapanda kitandani na kumlalia mtoto huyo, kinywa chake kikiwa juu ya kinywa cha mvulana huyo, macho yake juu ya macho yake, na viganja vyake juu ya viganja vyake, akaendelea kumlalia, na mwili wa mtoto huyo ukaanza kupata joto.+ 35 Kisha Elisha akatembea huku na kule chumbani, akapanda kitandani na kumlalia tena. Mvulana huyo akapiga chafya mara saba, kisha akafungua macho.+
-