-
Kutoka 14:21, 22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Sasa Musa akaunyoosha mkono wake juu ya bahari;+ naye Yehova akaisukuma bahari nyuma usiku kucha kwa upepo wenye nguvu wa mashariki, maji yakagawanyika,+ kukawa na nchi kavu+ katikati ya bahari. 22 Kwa hiyo Waisraeli wakapita kwenye nchi kavu katikati ya bahari,+ huku maji yakisimama kama ukuta upande wao wa kulia na wa kushoto.+
-
-
2 Wafalme 2:13, 14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Ndipo akaliokota vazi rasmi+ la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwa Eliya, akarudi na kusimama kwenye ukingo wa Yordani. 14 Kisha akachukua vazi rasmi la Eliya lililokuwa limeanguka kutoka kwake, akayapiga maji na kuuliza: “Yuko wapi Yehova, Mungu wa Eliya?” Alipoyapiga maji, yaligawanyika kushoto na kulia, Elisha akavuka ng’ambo.+
-