-
Kumbukumbu la Torati 3:13-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Kisha nusu ya kabila la Manase+ nimewapa sehemu inayobaki ya Gileadi na eneo lote la Bashani la ufalme wa Ogu. Eneo lote la Argobu, la Bashani, lilijulikana kuwa nchi ya Warefaimu.
14 “Yairi+ mwana wa Manase alichukua eneo lote la Argobu+ hadi kwenye mpaka wa Wageshuri na Wamaakathi,+ akaviita vijiji hivyo vya Bashani kwa jina lake mwenyewe, Hawoth-yairi,*+ mpaka leo. 15 Naye Makiri nimempa Gileadi.+ 16 Na watu wa kabila la Rubeni na kabila la Gadi+ nimewapa kuanzia Gileadi mpaka kwenye Bonde* la Arnoni, katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka, hadi Bonde la Yaboki, ambalo ni mpaka wa Waamoni,
-
-
Kumbukumbu la Torati 28:63Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
63 “Na kama Yehova alivyopendezwa wakati mmoja kuwafanikisha na kuwafanya mwongezeke, ndivyo Yehova atakavyopendezwa kuwaharibu na kuwaangamiza; nanyi mtang’olewa kutoka katika nchi mnayokaribia kuimiliki.
-
-
Yoshua 13:8-12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Nusu iliyobaki ya kabila la Manase, pamoja na watu wa kabila la Rubeni na Gadi walichukua urithi wao waliopewa na Musa upande wa mashariki wa Yordani, kama tu Musa mtumishi wa Yehova alivyowapa:+ 9 kuanzia Aroeri,+ kwenye ukingo wa Bonde* la Arnoni,+ na jiji lililo katikati ya bonde hilo, na uwanda wote wa juu wa Medeba hadi Diboni; 10 na majiji yote ya Mfalme Sihoni wa Waamori, aliyetawala Heshboni, hadi kwenye mpaka wa Waamoni;+ 11 pia Gileadi na eneo la Wageshuri na Wamaakathi+ na eneo lote la Mlima Hermoni na Bashani+ hadi Saleka;+ 12 ufalme wote wa Ogu kule Bashani, aliyetawala Ashtarothi na Edrei. (Alikuwa kati ya Warefaimu waliobaki.)+ Musa aliwashinda na kuwafukuza.*+
-