-
2 Mambo ya Nyakati 23:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Katika mwaka wa saba, Yehoyada alitenda kwa ujasiri na kufanya mapatano* na wakuu wa mamia,+ yaani, Azaria mwana wa Yerohamu, Ishmaeli mwana wa Yehohanani, Azaria mwana wa Obedi, Maaseya mwana wa Adaya, na Elishafati mwana wa Zikri. 2 Kisha wakazunguka katika nchi yote ya Yuda na kuwakusanya pamoja Walawi+ kutoka katika majiji yote ya Yuda na viongozi wa koo* za Waisraeli. Walipofika Yerusalemu, 3 kutaniko lote lilifanya agano+ pamoja na mfalme katika nyumba ya Mungu wa kweli, kisha akawaambia:
“Tazama! Mwana wa mfalme atatawala, kama Yehova alivyoahidi kuhusu wana wa Daudi.+
-