8 Sasa mwambie hivi mtumishi wangu Daudi: ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Nilikutoa malishoni, ili usiendelee kuchunga kondoo,+ uwe kiongozi wa watu wangu Waisraeli.+
12 Siku zako zitakapokwisha+ nawe ufe na kuzikwa pamoja na mababu zako, ndipo nitakapomwinua mzao wako* baada yako, mwana wako mwenyewe,* nami nitauimarisha kabisa ufalme wake.+
4 Na Yehova atatimiza ahadi aliyotoa kunihusu aliposema hivi: ‘Ikiwa wana wako wataikazia uangalifu njia yao kwa kutembea kwa uaminifu mbele zangu kwa moyo wao wote na kwa nafsi* yao yote,+ hutakosa kamwe mwanamume wa uzao wako atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.’+
5 ndipo nitakapoimarisha kiti chako cha ufalme juu ya Israeli milele, kama nilivyomwahidi Daudi baba yako, kwa kusema, ‘Hutakosa kamwe mwanamume wa uzao wako atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha Israeli.’+