3 “Nakusihi, Ee Yehova, tafadhali, kumbuka jinsi ambavyo nimetembea mbele zako kwa uaminifu na kwa moyo kamili, nami nimetenda mambo mema machoni pako.”+ Kisha Hezekia akaanza kulia sana na kububujikwa na machozi.
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano* mbele za Yehova,+ kwamba atamfuata Yehova na kushika amri zake, vikumbusho vyake, na sheria zake kwa moyo wake wote na kwa nafsi* yake yote kwa kutekeleza maneno ya agano hilo yaliyoandikwa katika kitabu hicho. Watu wote wakakubali agano hilo.+