Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 49:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Fimbo ya ufalme haitaondoka Yuda,+ wala fimbo ya kiongozi kutoka katikati ya miguu yake, mpaka Shilo* atakapokuja,+ na mataifa yatamtii.+

  • 1 Wafalme 8:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Yehova ametimiza ahadi hiyo aliyoitoa, kwa maana nimechukua mahali pa baba yangu Daudi na kuketi kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama Yehova alivyoahidi. Pia nimejenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli,+

  • 1 Mambo ya Nyakati 17:11-14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “‘“Siku zako zitakapokwisha nawe uzikwe pamoja na mababu zako, nitamwinua mzao wako* baada yako, mmoja wa wana wako,+ nami nitauimarisha kabisa ufalme wake.+ 12 Yeye ndiye atakayenijengea nyumba,+ nami nitakiimarisha kabisa kiti chake cha ufalme milele.+ 13 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu.+ Sitauondoa upendo wangu mshikamanifu kutoka kwake+ kama nilivyouondoa kutoka kwa yule aliyekutangulia.+ 14 Nitamfanya asimame katika nyumba yangu na katika ufalme wangu milele,+ na kiti chake cha ufalme kitadumu milele.”’”+

  • Zaburi 132:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Yehova amemwapia Daudi;

      Kwa hakika hatakosa kutimiza neno lake:

      “Mmoja wa wazao wako,*

      Nitamfanya aketi kwenye kiti chako cha ufalme.+

  • Isaya 9:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Kwa wingi wa utawala wake*

      Na amani, hakutakuwa na mwisho,+

      Kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na juu ya ufalme wake

      Ili kuuimarisha kabisa+ na kuutegemeza

      Kupitia haki+ na uadilifu,+

      Kuanzia sasa mpaka milele.

      Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.

  • Isaya 11:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Na tawi+ litakua kutoka kwenye kisiki cha Yese,+

      Na chipukizi+ kutoka kwenye mizizi yake litazaa matunda.

  • Mathayo 21:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Isitoshe umati uliomtangulia na wale waliomfuata waliendelea kupaza sauti: “Tunaomba umwokoe, Mwana wa Daudi!+ Amebarikiwa yule anayekuja katika jina la Yehova!*+ Tunaomba umwokoe, katika vilele vilivyo juu!”+

  • Mathayo 22:42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 “Mna maoni gani kuhusu Kristo? Ni mwana wa nani?” Wakamwambia: “Wa Daudi.”+

  • Luka 1:32, 33
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Huyo atakuwa mkuu+ naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi,+ na Yehova* Mungu atampa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake,+ 33 naye atatawala akiwa Mfalme juu ya nyumba ya Yakobo milele, na Ufalme wake hautakuwa na mwisho.”+

  • Yohana 7:42
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 42 Je, andiko halisemi kwamba Kristo atatoka katika uzao wa Daudi+ na atatoka Bethlehemu,+ kijiji alichoishi Daudi?”+

  • Matendo 2:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Kwa sababu alikuwa nabii na alijua kwamba Mungu alikuwa amemwapia kwa kiapo kwamba angemfanya mmoja wa wazao wake* aketi kwenye kiti chake cha ufalme,+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki