-
2 Samweli 7:12-17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Siku zako zitakapokwisha+ nawe ufe na kuzikwa pamoja na mababu zako, ndipo nitakapomwinua mzao wako* baada yako, mwana wako mwenyewe,* nami nitauimarisha kabisa ufalme wake.+ 13 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ nami nitakiimarisha kabisa kiti cha ufalme wake milele.+ 14 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu.+ Atakapokosea, nitamkaripia kwa fimbo ya wanadamu na kwa viboko vya wana wa binadamu.*+ 15 Upendo wangu mshikamanifu hautaondolewa kwake kama nilivyouondoa kwa Sauli,+ niliyemwondoa kutoka mbele yako. 16 Nyumba yako na ufalme wako utakuwa salama milele mbele yako; kiti chako cha ufalme kitaimarishwa kabisa milele.”’”+
17 Nathani akamwambia Daudi maneno hayo yote na maono hayo yote.+
-