Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 8:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Na sasa, Ee Yehova Mungu wa Israeli, timiza ahadi uliyomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu ulipomwambia, ‘Hutakosa kamwe mwanamume wa uzao wako atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha Israeli mbele zangu, ikiwa tu wana wako watakazia uangalifu njia yao kwa kutembea mbele zangu, kama ulivyotembea mbele zangu.’+

  • Zaburi 89:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 “Nimefanya agano pamoja na yule niliyemchagua;+

      Nimemwapia Daudi mtumishi wangu:+

       4 ‘Nitauimarisha kabisa uzao wako*+ milele,

      Nami nitakijenga kiti chako cha ufalme kwa vizazi vyote.’”+ (Sela)

  • Zaburi 89:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Nimempata Daudi mtumishi wangu;+

      Kwa mafuta yangu matakatifu nimemtia mafuta.+

  • Zaburi 89:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Uzao wake utadumu* milele;+

      Kiti chake cha ufalme kitadumu kama jua mbele zangu.+

  • Isaya 9:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Kwa wingi wa utawala wake*

      Na amani, hakutakuwa na mwisho,+

      Kwenye kiti cha ufalme cha Daudi+ na juu ya ufalme wake

      Ili kuuimarisha kabisa+ na kuutegemeza

      Kupitia haki+ na uadilifu,+

      Kuanzia sasa mpaka milele.

      Bidii ya Yehova wa majeshi itafanya hayo.

  • Yeremia 33:20, 21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 “Yehova anasema hivi, ‘Ikiwa mngeweza kulivunja agano langu kuhusu mchana na agano langu kuhusu usiku, ili kuzuia mchana na usiku usije kwa wakati wake,+ 21 hapo ndipo agano langu pamoja na mtumishi wangu Daudi lingeweza kuvunjwa,+ ili asiwe na mwana anayetawala akiwa mfalme kwenye kiti chake cha ufalme,+ na pia agano langu pamoja na makuhani, Walawi, wahudumu wangu.+

  • Mathayo 9:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Yesu alipokuwa akitoka huko, wanaume wawili vipofu+ wakamfuata, wakipaza sauti: “Tuhurumie,* Mwana wa Daudi.”

  • Luka 1:69
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 69 Naye ametuinulia pembe ya wokovu*+ katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,+

  • Matendo 2:30, 31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Kwa sababu alikuwa nabii na alijua kwamba Mungu alikuwa amemwapia kwa kiapo kwamba angemfanya mmoja wa wazao wake* aketi kwenye kiti chake cha ufalme,+ 31 aliona mapema na kusema kuhusu ufufuo wa Kristo, kwamba hakuachwa katika Kaburi* wala mwili wake haukuona uharibifu.*+

  • Matendo 13:22, 23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Baada ya kumwondoa, akamwinua Daudi awe mfalme wao,+ na akatoa ushahidi kumhusu akisema: ‘Nimempata Daudi mwana wa Yese,+ mtu anayeupendeza moyo wangu;+ atafanya mambo yote ninayotamani.’ 23 Kama alivyoahidi, kutoka katika uzao wa* mwanamume huyu, Mungu amewaletea Israeli mwokozi, yaani, Yesu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki