-
Yeremia 31:35-37Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
35 Yehova,
Ambaye hutoa jua ili liangaze wakati wa mchana,
Sheria za* mwezi na nyota ili ziangaze usiku,
Anayeitibua bahari na kuyavuruga mawimbi yake,
Ambaye jina lake ni Yehova wa majeshi, anasema hivi:+
36 “‘Ikiwa sheria hizo zitakoma,’ asema Yehova,
‘Basi uzao wa Israeli utakoma daima kuwa taifa mbele zangu.’”+
37 Yehova anasema hivi: “‘Ikiwa mbingu zilizo juu zinaweza kupimwa na misingi ya dunia iliyo chini kuchunguzwa, basi ninaweza kuukataa uzao wote wa Israeli kwa sababu ya yote ambayo wamefanya,’ asema Yehova.”+
-