-
2 Wafalme 23:4, 5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Halafu mfalme akamwagiza kuhani mkuu Hilkia,+ makuhani wa daraja la pili, na walinzi wa milango waondoe kutoka katika hekalu la Yehova vyombo vyote vilivyotengenezwa kwa ajili ya Baali, kwa ajili ya mti mtakatifu,*+ na kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni. Kisha akaviteketeza nje ya Yerusalemu kwenye matuta ya Kidroni, akapeleka majivu yake Betheli.+ 5 Basi akawaondoa kabisa makuhani wa miungu ya kigeni, waliochaguliwa na wafalme wa Yuda kufukiza moshi wa dhabihu mahali pa juu katika majiji ya Yuda na maeneo yanayozunguka Yerusalemu, na pia wale waliofukiza moshi wa dhabihu kwa Baali, kwa jua, kwa mwezi, kwa makundi ya nyota za unajimu, na kwa jeshi lote la mbinguni.+
-