-
2 Mambo ya Nyakati 33:7-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Sanamu aliyokuwa amechonga aliiweka katika nyumba ya Mungu wa kweli+ ambayo Mungu alikuwa amemwambia hivi Daudi na Sulemani mwanawe kuihusu: “Nitaweka jina langu milele katika nyumba hii na katika jiji la Yerusalemu, ambalo nimelichagua kati ya makabila yote ya Israeli.+ 8 Ikiwa Waisraeli watashika kwa uangalifu mambo yote niliyowaamuru, Sheria yote, masharti na amri nilizowapa* kupitia Musa mtumishi wangu, sitaiondoa tena kamwe miguu yao katika nchi niliyowapa mababu zao.” 9 Manase aliendelea kuwapotosha watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalemu, akasababisha watende mambo maovu zaidi kuliko mataifa ambayo Yehova alikuwa ameyaangamiza kutoka mbele ya Waisraeli.+
-