-
1 Wafalme 7:16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Naye alitumia shaba iliyoyeyushwa kutengeneza vifuniko viwili ambavyo vingewekwa juu ya nguzo hizo. Kifuniko kimoja kilikuwa na urefu wa mikono mitano, na kingine kilikuwa na urefu wa mikono mitano.
-
-
Yeremia 52:21-23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Kuhusu nguzo, kila nguzo ilikuwa na kimo cha mikono 18,* na kamba ya kupimia yenye urefu wa mikono 12 ingeweza kuizunguka;+ unene wake ulikuwa upana wa vidole vinne,* na ndani ilikuwa wazi. 22 Na kifuniko cha nguzo kilikuwa cha shaba; na urefu wa kila kifuniko ulikuwa mikono mitano;+ na wavu pamoja na makomamanga yote yaliyozunguka kifuniko hicho yalitengenezwa kwa shaba. Nguzo ya pili ilifanana na nguzo ya kwanza, pia yale makomamanga. 23 Kulikuwa na makomamanga 96 kandokando; jumla, kulikuwa na makomamanga 100 kuzunguka ule wavu.+
-