-
1 Wafalme 7:15-20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Alitengeneza nguzo mbili kwa kutumia shaba iliyoyeyushwa;+ kila nguzo ilikuwa na urefu wa mikono 18, na kila moja ya nguzo hizo mbili ingeweza kuzungukwa kwa kamba yenye urefu wa mikono 12.*+ 16 Naye alitumia shaba iliyoyeyushwa kutengeneza vifuniko viwili ambavyo vingewekwa juu ya nguzo hizo. Kifuniko kimoja kilikuwa na urefu wa mikono mitano, na kingine kilikuwa na urefu wa mikono mitano. 17 Kifuniko cha kila nguzo kilikuwa na wavu uliofumwa wa minyororo;+ nguzo moja ilikuwa na nyavu saba na nguzo nyingine nyavu saba. 18 Naye alitengeneza safu mbili za makomamanga kuzunguka wavu uliofunika vifuniko vilivyokuwa juu ya nguzo; alifanya hivyo kwa kila nguzo. 19 Vifuniko vilivyokuwa juu ya nguzo za ukumbi vilikuwa na umbo la yungiyungi, na urefu wake ulikuwa mikono minne. 20 Vifuniko hivyo vilikuwa juu ya zile nguzo mbili, juu tu ya sehemu ya mviringo iliyoungana na zile nyavu; na kulikuwa na safu za makomamanga 200 kuzunguka kila kifuniko cha nguzo.+
-