-
1 Wafalme 8:63, 64Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
63 Sulemani alimtolea Yehova dhabihu za ushirika:+ Alitoa ng’ombe 22,000 na kondoo 120,000. Basi mfalme na Waisraeli wote wakaizindua nyumba ya Yehova.+ 64 Siku hiyo ilimbidi mfalme atakase sehemu ya katikati ya ua ulio mbele ya nyumba ya Yehova, kwa sababu alipaswa kutolea mahali hapo dhabihu za kuteketezwa, matoleo ya nafaka, na vipande vya mafuta vya dhabihu za ushirika, kwa sababu madhabahu ya shaba+ iliyo mbele za Yehova ilikuwa ndogo sana isiweze kutoshea dhabihu za kuteketezwa, matoleo ya nafaka, na vipande vya mafuta+ vya dhabihu za ushirika.
-