-
2 Samweli 6:17-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Basi wakaliingiza ndani Sanduku la Yehova na kuliweka mahali pake ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amepiga ili aliweke humo.+ Kisha Daudi akatoa dhabihu za kuteketezwa+ na dhabihu za ushirika+ mbele za Yehova.+ 18 Daudi alipomaliza kutoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika, akawabariki watu katika jina la Yehova wa majeshi. 19 Pia, akawagawia watu wote, umati wote wa Waisraeli, kila mwanamume na mwanamke mkate wa mviringo, keki ya tende, na keki ya zabibu kavu, halafu watu wote wakaenda zao, kila mmoja nyumbani kwake mwenyewe.
-