-
1 Mambo ya Nyakati 16:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
16 Basi wakaliingiza Sanduku la Mungu wa kweli na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amepiga ili aliweke humo;+ nao wakatoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika mbele za Mungu wa kweli.+ 2 Daudi alipomaliza kutoa dhabihu za kuteketezwa+ na dhabihu za ushirika,+ akawabariki watu katika jina la Yehova. 3 Isitoshe, aliwagawia Waisraeli wote, kila mwanamume na mwanamke, mkate mmoja wa mviringo, keki ya tende, na keki ya zabibu kavu.
-