25Isitoshe, Daudi na wakuu wa vikundi vya utumishi waliwatenga baadhi ya wana wa Asafu, Hemani, na Yeduthuni+ ili watoe unabii kwa kutumia vinubi, vinanda,+ na matoazi.+ Hii ndiyo orodha ya wanaume waliowekwa rasmi kwa ajili ya utumishi huo:
3 Kutoka kwa Yeduthuni,+ wana wa Yeduthuni walikuwa: Gedalia, Zeri, Yeshaya, Shimei, Hashabia, na Matithia,+ wana sita, waliokuwa chini ya usimamizi wa Yeduthuni baba yao, aliyetoa unabii kwa kutumia kinubi, akimshukuru na kumsifu Yehova.+