-
1 Mambo ya Nyakati 16:41, 42Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
41 Walikuwa pamoja na Hemani na Yeduthuni+ na wanaume wengine waliochaguliwa na kutajwa majina ili wamshukuru Yehova,+ kwa sababu “upendo wake mshikamanifu unadumu milele”;+ 42 nao walikuwa pamoja na Hemani+ na Yeduthuni ili wapige tarumbeta, matoazi, na ala zilizotumiwa kumsifu* Mungu wa kweli; na wana wa Yeduthuni+ walikuwa langoni.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 5:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Makuhani walipotoka mahali patakatifu (kwa maana makuhani wote waliokuwepo walikuwa wamejitakasa,+ bila kuzingatia vikundi vyao),+ 12 waimbaji wote Walawi+ walioongozwa na Asafu,+ Hemani,+ Yeduthuni,+ wana wao na ndugu zao walikuwa wamevaa mavazi ya kitambaa bora, wakiwa wamebeba matoazi, vinanda, na vinubi; walikuwa wamesimama upande wa mashariki wa madhabahu, na makuhani 120 waliokuwa wakipiga tarumbeta walikuwa pamoja nao.+
-