Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Samweli 7:4-7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Usiku huohuo, neno hili la Yehova likamjia Nathani: 5 “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Je, utanijengea nyumba nikae ndani yake?+ 6 Kwa maana sijakaa ndani ya nyumba tangu siku nilipowatoa watu wa Israeli huko Misri mpaka leo,+ bali nimekuwa nikihama* huku na kule katika hema na katika hema la ibada.+ 7 Wakati wote nilipotembea na Waisraeli wote,* je, niliwahi wakati wowote kumuuliza kiongozi yeyote wa kabila la Israeli niliyemweka awachunge watu wangu Waisraeli, ‘Kwa nini hukunijengea nyumba ya mierezi?’”’

  • 1 Wafalme 8:17-19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Moyo wa baba yangu Daudi ulitamani kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli.+ 18 Lakini Yehova akamwambia Daudi baba yangu, ‘Moyo wako ulitamani kujenga nyumba kwa ajili ya jina langu, na ulifanya vizuri kutamani jambo hilo moyoni mwako. 19 Hata hivyo, hutajenga nyumba hiyo, lakini mwana wako mwenyewe utakayemzaa* ndiye atakayeijenga nyumba hiyo kwa ajili ya jina langu.’+

  • 1 Mambo ya Nyakati 22:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Daudi alimwambia hivi Sulemani mwanawe: “Moyo wangu ulitamani kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wangu.+ 8 Lakini neno la Yehova lilinijia likisema, ‘Umemwaga damu nyingi sana, nawe umepigana vita vikubwa. Hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ kwa maana umemwaga damu nyingi sana duniani mbele zangu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki