Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 5:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 “Unajua vizuri kwamba baba yangu Daudi hakuweza kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wake kwa sababu ya watu waliopigana vita naye pande zote, mpaka Yehova alipowaweka maadui wake chini ya nyayo za miguu yake.+

  • 1 Wafalme 8:17-19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Moyo wa baba yangu Daudi ulitamani kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wa Israeli.+ 18 Lakini Yehova akamwambia Daudi baba yangu, ‘Moyo wako ulitamani kujenga nyumba kwa ajili ya jina langu, na ulifanya vizuri kutamani jambo hilo moyoni mwako. 19 Hata hivyo, hutajenga nyumba hiyo, lakini mwana wako mwenyewe utakayemzaa* ndiye atakayeijenga nyumba hiyo kwa ajili ya jina langu.’+

  • 1 Mambo ya Nyakati 17:4-6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Yehova anasema hivi: “Si wewe utakayenijengea nyumba nitakayokaa ndani yake.+ 5 Kwa maana sijakaa ndani ya nyumba tangu siku nilipowatoa nje Waisraeli mpaka leo, bali nimekuwa nikihama hema moja hadi hema lingine na kutoka hema moja la ibada hadi hema lingine la ibada.*+ 6 Wakati wote nilipotembea na Waisraeli wote, je, niliwahi wakati wowote kumuuliza mwamuzi yeyote wa Israeli niliyemweka awachunge watu wangu, ‘Kwa nini hukunijengea nyumba ya mierezi?’”’

  • 1 Mambo ya Nyakati 22:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Daudi alimwambia hivi Sulemani mwanawe: “Moyo wangu ulitamani kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Yehova Mungu wangu.+ 8 Lakini neno la Yehova lilinijia likisema, ‘Umemwaga damu nyingi sana, nawe umepigana vita vikubwa. Hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu,+ kwa maana umemwaga damu nyingi sana duniani mbele zangu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki