-
2 Samweli 24:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Hasira ya Yehova ikawaka tena dhidi ya Waisraeli+ mtu fulani alipomchochea Daudi* atende kinyume chao kwa kumwambia: “Nenda, ukawahesabu+ watu wa Israeli na Yuda.”+ 2 Basi mfalme akamwambia Yoabu+ mkuu wa jeshi aliyekuwa pamoja naye: “Tafadhali nenda katika makabila yote ya Israeli, kuanzia Dani mpaka Beer-sheba,+ uwaandikishe watu, ili nijue idadi yao.” 3 Lakini Yoabu akamwambia mfalme: “Yehova Mungu wako na azidishe idadi ya watu mara 100, na macho yako bwana wangu mfalme na yaone jambo hilo, lakini kwa nini bwana wangu mfalme unataka kufanya jambo la namna hii?”
-