-
1 Mambo ya Nyakati 21:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Kisha Shetani* akasimama dhidi ya Waisraeli na kumchochea Daudi awahesabu Waisraeli.+ 2 Basi Daudi akamwambia Yoabu+ na wakuu wa watu: “Nendeni mkawahesabu Waisraeli kuanzia Beer-sheba mpaka Dani;+ kisha mniletee habari ili nijue idadi yao.” 3 Lakini Yoabu akasema: “Yehova na azidishe idadi ya watu wake mara 100! Bwana wangu mfalme, hao wote tayari ni watumishi wako bwana wangu, sivyo? Kwa nini bwana wangu unataka kufanya hivyo? Kwa nini uwafanye Waisraeli wawe na hatia?”
-