-
Hesabu 31:50Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
50 Kwa hiyo mruhusu kila mmoja wetu atoe vitu alivyopata ili viwe vya Yehova, yaani, vitu vya dhahabu, mikufu ya miguuni, bangili, pete za muhuri, vipuli, na vito vingine, ili Yehova afunike dhambi zetu.”
-
-
1 Mambo ya Nyakati 18:10, 11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 mara moja alimtuma Hadoramu mwana wake kwa Mfalme Daudi ili amjulie hali na kumpongeza kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumshinda (kwa maana mara nyingi Hadadezeri alimshambulia Tou), na Hadoramu alimletea Daudi kila aina ya vitu vya dhahabu, fedha, na shaba. 11 Mfalme Daudi akavitakasa vitu hivyo ili viwe vya Yehova,+ pamoja na fedha na dhahabu aliyokuwa amechukua kutoka kwa mataifa yote: kutoka kwa Waedomu na Wamoabu, kutoka kwa Waamoni,+ Wafilisti,+ na Waamaleki.+
-