-
2 Wafalme 12:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Waliwapa wale waliowekwa kusimamia kazi katika nyumba ya Yehova pesa zilizokuwa zimehesabiwa. Nao wakawalipa maseremala na wajenzi waliokuwa wakifanya kazi katika nyumba ya Yehova,+ 12 na pia waashi na watu waliokata mawe. Pia walinunua mbao na mawe yaliyochongwa kwa ajili ya kurekebisha sehemu zilizoharibika za nyumba ya Yehova na kutumia pesa hizo kulipia gharama nyingine zote za kurekebisha nyumba hiyo.
-