30Hezekia akatuma ujumbe kwa watu wote wa Israeli+ na Yuda, na hata aliwaandikia barua watu wa Efraimu na Manase+ waje Yerusalemu katika nyumba ya Yehova kuadhimisha Pasaka ya Yehova Mungu wa Israeli.+
12 Mkono wa Mungu wa kweli ulikuwa pia juu ya watu wa Yuda ili kuwaunganisha* watekeleze yale ambayo mfalme na wakuu walikuwa wameamuru kulingana na neno la Yehova.
16 Aliitayarisha pia madhabahu ya Yehova,+ akaanza kutoa juu yake dhabihu za ushirika+ na dhabihu za shukrani,+ naye akawaambia watu wa Yuda wamtumikie Yehova Mungu wa Israeli.