Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 25:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Utazitia fito hizo katika zile pete zilizo kwenye pande mbili za Sanduku ili zitumiwe kulibeba.

  • Hesabu 4:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 “Ni lazima Haruni na wanawe wamalize kufunika mahali patakatifu+ na vyombo vyote vya mahali patakatifu kabla ya watu kuanza safari. Kisha wana wa Kohathi watakuja kuvibeba,+ lakini hawapaswi kugusa vitu vitakatifu, la sivyo watakufa.+ Wana wa Kohathi ndio walio na jukumu la kubeba vitu vya hema la mkutano.

  • 1 Wafalme 8:3-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Basi wazee wote wa Israeli wakaja, na makuhani wakalibeba Sanduku.+ 4 Wakalipandisha kutoka huko Sanduku la Yehova, hema la mkutano,+ na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa katika hema hilo. Makuhani na Walawi wakavipandisha vitu hivyo. 5 Mfalme Sulemani na Waisraeli wote waliokusanywa ili wakutane naye, walikuwa mbele ya Sanduku. Kondoo na ng’ombe wengi sana wasiohesabika au kujulikana idadi walikuwa wakitolewa dhabihu.+

  • 1 Mambo ya Nyakati 15:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Huo ndio wakati ambao Daudi alisema: “Hakuna mtu yeyote anayepaswa kubeba Sanduku la Mungu wa kweli isipokuwa Walawi, kwa maana Yehova amewachagua ili walibebe Sanduku la Yehova na kumhudumia sikuzote.”+

  • 1 Mambo ya Nyakati 15:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Kisha Walawi wakalibeba Sanduku la Mungu wa kweli mabegani mwao kwa kutumia fito zake,+ kama Musa alivyoamuru kwa neno la Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki