-
Kutoka 25:14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
14 Utazitia fito hizo katika zile pete zilizo kwenye pande mbili za Sanduku ili zitumiwe kulibeba.
-
-
Hesabu 4:15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 “Ni lazima Haruni na wanawe wamalize kufunika mahali patakatifu+ na vyombo vyote vya mahali patakatifu kabla ya watu kuanza safari. Kisha wana wa Kohathi watakuja kuvibeba,+ lakini hawapaswi kugusa vitu vitakatifu, la sivyo watakufa.+ Wana wa Kohathi ndio walio na jukumu la kubeba vitu vya hema la mkutano.
-
-
1 Wafalme 8:3-5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Basi wazee wote wa Israeli wakaja, na makuhani wakalibeba Sanduku.+ 4 Wakalipandisha kutoka huko Sanduku la Yehova, hema la mkutano,+ na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa katika hema hilo. Makuhani na Walawi wakavipandisha vitu hivyo. 5 Mfalme Sulemani na Waisraeli wote waliokusanywa ili wakutane naye, walikuwa mbele ya Sanduku. Kondoo na ng’ombe wengi sana wasiohesabika au kujulikana idadi walikuwa wakitolewa dhabihu.+
-