-
2 Mambo ya Nyakati 5:4-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Basi wazee wote wa Israeli wakaja, na Walawi wakalibeba Sanduku.+ 5 Wakalipandisha Sanduku, hema la mkutano,+ na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa katika hema hilo. Makuhani na Walawi* wakavipandisha vitu hivyo. 6 Mfalme Sulemani na Waisraeli wote waliokusanywa ili wakutane naye walikuwa mbele ya Sanduku. Kondoo na ng’ombe wengi sana wasiohesabika au kujulikana idadi walikuwa wakitolewa dhabihu.+
-