-
2 Mambo ya Nyakati 15:8, 9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Mara tu Asa aliposikia maneno hayo na unabii wa nabii Odedi, akajipa ujasiri, akaondoa sanamu zenye kuchukiza katika nchi yote ya Yuda+ na Benjamini na katika majiji aliyokuwa ameteka katika eneo lenye milima la Efraimu, naye akajenga upya madhabahu ya Yehova iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Yehova.+ 9 Akawakusanya pamoja watu wote wa Yuda na Benjamini na wakaaji wageni waliokuwa pamoja nao kutoka Efraimu na Manase na Simeoni,+ kwa maana walikuwa wamekimbia na kuja kwake kwa wingi kutoka Israeli walipoona kwamba Yehova Mungu wake alikuwa pamoja naye.
-