Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 12:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Mtaleta vitu vyote ninavyowaamuru mahali ambapo Yehova Mungu wenu atachagua jina lake likae hapo+—dhabihu zenu za kuteketezwa, matoleo yenu, sehemu zenu za kumi,+ mchango kutoka mkononi mwenu, na kila dhabihu ya nadhiri mnayoweka nadhiri kwa Yehova.

  • 1 Mambo ya Nyakati 22:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Ndipo Daudi akasema: “Hii ndiyo nyumba ya Yehova Mungu wa kweli, na hii ndiyo madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa kwa ajili ya Waisraeli.”+

  • 2 Mambo ya Nyakati 15:8, 9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Mara tu Asa aliposikia maneno hayo na unabii wa nabii Odedi, akajipa ujasiri, akaondoa sanamu zenye kuchukiza katika nchi yote ya Yuda+ na Benjamini na katika majiji aliyokuwa ameteka katika eneo lenye milima la Efraimu, naye akajenga upya madhabahu ya Yehova iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Yehova.+ 9 Akawakusanya pamoja watu wote wa Yuda na Benjamini na wakaaji wageni waliokuwa pamoja nao kutoka Efraimu na Manase na Simeoni,+ kwa maana walikuwa wamekimbia na kuja kwake kwa wingi kutoka Israeli walipoona kwamba Yehova Mungu wake alikuwa pamoja naye.

  • 2 Mambo ya Nyakati 30:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kwa hiyo wajumbe* hao walienda jiji hadi jiji katika nchi yote ya Efraimu na Manase,+ walifika hata Zabuloni, lakini watu walikuwa wakiwafanyia mzaha na kuwadhihaki.+ 11 Hata hivyo, watu fulani kutoka Asheri, Manase, na Zabuloni walijinyenyekeza na kuja Yerusalemu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki