38 Akatumia mbao za mshita kutengeneza madhabahu ya dhabihu za kuteketezwa. Ilikuwa ya mraba, yenye urefu wa mikono mitano, upana wa mikono mitano, na kimo cha mikono mitatu.+ 2 Kisha akatengeneza pembe kwenye ncha zake nne. Pembe hizo zilikuwa sehemu ya hiyo madhabahu. Naye akaifunika kwa shaba.+