-
1 Wafalme 7:13, 14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Mfalme Sulemani akawatuma watu wamwite Hiramu,+ akaletwa kutoka Tiro. 14 Alikuwa mwana wa mwanamke mjane kutoka katika kabila la Naftali, na baba yake alikuwa mfua shaba+ kutoka Tiro; Hiramu alikuwa na ustadi wa hali ya juu, uelewaji,+ na uzoefu wa kutengeneza vitu vya shaba vya kila aina. Basi akaja kwa Mfalme Sulemani na kufanya kazi yake yote.
-
-
2 Mambo ya Nyakati 4:11-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Hiramu alitengeneza pia ndoo za kuondolea majivu, pia sepetu, na mabakuli.+
Basi Hiramu akamaliza kazi yote aliyomfanyia Mfalme Sulemani kuhusiana na nyumba ya Mungu wa kweli:+ 12 zile nguzo mbili+ na vifuniko vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya nguzo hizo; na nyavu mbili+ za kufunika vifuniko hivyo viwili vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya nguzo hizo; 13 yale makomamanga 400+ kwa ajili ya zile nyavu mbili, safu mbili za makomamanga kwa ajili ya kila wavu, ili kufunika vile vifuniko viwili vyenye umbo la bakuli vilivyokuwa juu ya zile nguzo;+ 14 yale magari* kumi na yale mabeseni kumi yaliyokuwa juu ya magari hayo;+ 15 ile Bahari na wale ng’ombe dume 12 waliokuwa chini yake;+ 16 na ndoo za kuondolea majivu, sepetu, nyuma,*+ na vyombo vingine vyote ambavyo Hiram-abivu+ alimtengenezea Mfalme Sulemani kwa shaba iliyong’arishwa kwa ajili ya nyumba ya Yehova.
-