-
1 Wafalme 15:17-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Basi Mfalme Baasha wa Israeli alikuja kushambulia Yuda, akaanza kujenga* Rama+ ili kumzuia mtu yeyote asitoke wala kuingia kwa* Mfalme Asa wa Yuda.+ 18 Ndipo Asa akachukua fedha yote na dhahabu iliyokuwa imebaki katika hazina za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya* mfalme na kuwapa watumishi wake. Kisha Mfalme Asa akawatuma kwa Ben-hadadi mwana wa Tabrimoni mwana wa Hezioni, mfalme wa Siria,+ aliyekuwa akiishi Damasko, akamwambia: 19 “Kuna mkataba* kati yangu na wewe na kati ya baba yangu na baba yako. Ninakutumia zawadi ya fedha na dhahabu. Njoo, vunja mkataba wako* na Mfalme Baasha wa Israeli, ili aondoke kwangu.”
-