-
1 Wafalme 22:19-23Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Ndipo Mikaya akasema: “Basi, sikia neno la Yehova: Nilimwona Yehova akiwa ameketi kwenye kiti chake cha ufalme+ na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kando yake, upande wake wa kulia na upande wake wa kushoto.+ 20 Halafu Yehova akauliza, ‘Ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili apande kwenda na kufia huko Ramothi-gileadi?’ Na malaika mmoja akasema jambo moja na mwingine akasema jambo lingine. 21 Kisha roho*+ fulani akaja na kusimama mbele za Yehova na kusema, ‘Mimi nitamdanganya.’ Yehova akamuuliza, ‘Utatumia njia gani?’ 22 Akajibu, ‘Nitaenda na kuwa roho ya udanganyifu katika vinywa vya manabii wake wote.’+ Kwa hiyo akasema, ‘Utamdanganya, na zaidi ya hilo, utafanikiwa. Nenda ukafanye hivyo.’ 23 Na sasa Yehova ametia roho ya udanganyifu katika vinywa vya hawa manabii wako wote,+ lakini Yehova ametangaza kwamba utapata msiba.”+
-