-
2 Mambo ya Nyakati 18:18-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Ndipo Mikaya akasema: “Basi, sikia neno la Yehova: Nilimwona Yehova akiwa ameketi kwenye kiti chake cha ufalme+ na jeshi lote la mbinguni+ likiwa limesimama upande wake wa kulia na upande wake wa kushoto.+ 19 Halafu Yehova akauliza, ‘Ni nani atakayemdanganya Mfalme Ahabu wa Israeli, ili apande kwenda na kufia huko Ramothi-gileadi?’ Na malaika mmoja akasema jambo moja na mwingine akasema jambo lingine. 20 Kisha roho*+ fulani akaja na kusimama mbele za Yehova na kusema, ‘Mimi nitamdanganya.’ Yehova akamuuliza, ‘Utatumia njia gani?’ 21 Akajibu, ‘Nitaenda na kuwa roho ya udanganyifu katika vinywa vya manabii wake wote.’ Kwa hiyo akasema, ‘Utamdanganya, na zaidi ya hilo, utafanikiwa. Nenda ukafanye hivyo.’ 22 Na sasa Yehova ametia roho ya udanganyifu katika vinywa vya hawa manabii wako,+ lakini Yehova ametangaza kwamba utapata msiba.”
-
-
Danieli 7:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 “Nikaendelea kutazama mpaka viti vya ufalme vikawekwa na Mzee wa Siku+ akaketi.+ Mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji,+ na nywele za kichwa chake zilikuwa kama sufu safi. Kiti chake cha ufalme kilikuwa miali ya moto; magurudumu yake yalikuwa moto unaowaka.+ 10 Mto wa moto ulikuwa ukitiririka kutoka mbele zake.+ Elfu kwa maelfu waliendelea kumhudumia, na elfu kumi mara elfu kumi walisimama mbele zake.+ Mahakama+ ikaketi, na vitabu vikafunguliwa.
-