-
Kutoka 30:12-16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 “Wakati wowote unapowahesabu wana wa Israeli,+ ni lazima kila mmoja wao anipe mimi Yehova fidia kwa ajili ya nafsi yake* watu wanapohesabiwa. Watafanya hivyo ili wasipatwe na pigo lolote wanapoandikishwa. 13 Wote watakaoandikishwa watatoa nusu ya shekeli* kulingana na shekeli ya kawaida ya mahali patakatifu.*+ Gera 20* ni sawa na shekeli moja. Nusu shekeli ni mchango kwa Yehova.+ 14 Kila mtu mwenye umri wa kuanzia miaka 20 anayeandikishwa atatoa mchango wa Yehova.+ 15 Tajiri hapaswi kutoa zaidi na maskini hapaswi kutoa mchango wa Yehova unaopungua nusu shekeli* ili kutoa dhabihu ya kufunika dhambi kwa ajili ya nafsi zenu.* 16 Unapaswa kuchukua kutoka kwa Waisraeli fedha za dhabihu ya kufunika dhambi na kuzitoa ili zitumiwe katika utumishi wa hema la mkutano, ziwe kumbukumbu mbele za Yehova kwa ajili ya Waisraeli, ili kufunika dhambi kwa ajili ya nafsi zenu.”*
-