Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 14:1-6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Mfalme Yehoashi wa Yuda akawa mfalme. 2 Alikuwa na umri wa miaka 25 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 29 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Yehoadini wa Yerusalemu.+ 3 Aliendelea kutenda yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, lakini si kama Daudi+ babu yake. Alifanya mambo yote kama Yehoashi baba yake.+ 4 Hata hivyo, mahali pa juu hapakuondolewa,+ na watu bado walikuwa wakitoa dhabihu na kufukiza moshi wa dhabihu katika mahali pa juu.+ 5 Mara tu ufalme ulipoimarika kabisa mikononi mwake, aliwaua watumishi wake waliomuua mfalme, baba yake.+ 6 Lakini hakuwaua wana wa wauaji hao, kulingana na amri hii ya Yehova iliyoandikwa katika kitabu cha Sheria ya Musa: “Akina baba hawapaswi kuuawa kwa sababu ya wana wao, na wana hawapaswi kuuawa kwa sababu ya baba zao; lakini kila mtu anapaswa kuuawa kwa sababu ya dhambi yake mwenyewe.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki