4 Kisha shujaa mmoja akatoka katika kambi za Wafilisti; aliitwa Goliathi,+ kutoka Gathi,+ alikuwa na urefu wa mikono sita na shubiri moja. 5 Alikuwa na kofia ya shaba kichwani, naye alivaa koti la vita lenye magamba yanayolaliana. Koti hilo la vita la shaba+ lilikuwa na uzito wa shekeli 5,000.