-
1 Wafalme 7:23-26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
23 Kisha akatengeneza Bahari* kwa madini yaliyoyeyushwa.+ Ilikuwa ya mviringo, yenye upana wa mikono 10 ukingo hadi ukingo na kimo cha mikono 5, na ingeweza kuzungukwa na kamba yenye urefu wa mikono 30.*+ 24 Na chini ya ukingo wake kulikuwa na mapambo ya vibuyu,+ nayo yalizunguka ukingo wote, vibuyu kumi kwa kila mkono mmoja kuzunguka Bahari yote, na safu mbili za vibuyu zilitengenezwa kwa kuyeyushwa zikiwa sehemu ya Bahari hiyo. 25 Ilikuwa juu ya ng’ombe dume 12,+ watatu wakitazama kaskazini, watatu wakitazama magharibi, watatu wakitazama kusini, na watatu wakitazama mashariki; na Bahari hiyo ilikuwa juu yao, na sehemu zao zote za nyuma zilielekea katikati. 26 Na unene wake ulikuwa upana wa kiganja kimoja;* na ukingo wake ulitengenezwa kama ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi. Ingeweza kujaa maji kiasi cha bathi 2,000.*
-