-
1 Wafalme 8:65, 66Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
65 Wakati huo Sulemani alifanya sherehe hiyo+ pamoja na Waisraeli wote, kutaniko kubwa kuanzia Lebo-hamathi* na kushuka mpaka kwenye Korongo* la Misri,+ mbele za Yehova Mungu wetu kwa siku 7 na kisha siku nyingine 7, jumla ya siku 14. 66 Siku iliyofuata,* aliwaruhusu watu waondoke, nao wakambariki mfalme na kwenda nyumbani kwao wakishangilia na kufurahi moyoni kwa sababu ya wema wote+ ambao Yehova alikuwa amemtendea Daudi mtumishi wake na watu wake Waisraeli.
-