-
Ezra 5:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
5 Ndipo nabii Hagai+ na nabii Zekaria,+ mjukuu wa Ido+ wakawatabiria Wayahudi waliokuwa Yuda na Yerusalemu, katika jina la Mungu wa Israeli aliyekuwa akiwaongoza. 2 Kisha Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli na Yeshua+ mwana wa Yehosadaki wakaanza kujenga upya nyumba ya Mungu,+ iliyokuwa Yerusalemu; na manabii wa Mungu walikuwa pamoja nao na waliwatia moyo.+
-
-
Zekaria 6:15Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Na wale walio mbali sana watakuja na kushiriki katika ujenzi wa hekalu la Yehova.” Nanyi mtalazimika kujua kwamba Yehova wa majeshi amenituma kwenu. Na itakuwa hivyo—ikiwa hamtakosa kuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu.’”
-