Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 23:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Hampaswi kufanya agano pamoja nao wala na miungu yao.+

  • Kutoka 34:15, 16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Muwe waangalifu msifanye agano na wakaaji wa nchi, kwa maana wanapofanya ukahaba na miungu yao na kuitolea dhabihu,+ mmoja wao atawaalika nanyi mtakula dhabihu yake.+ 16 Kisha kwa hakika mtawachukua baadhi ya mabinti wao ili waolewe na wana wenu,+ na mabinti wao watafanya ukahaba na miungu yao na kusababisha wana wenu wafanye ukahaba na miungu yao.+

  • Kumbukumbu la Torati 7:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Msioane nao kamwe. Msikubali mabinti wenu waolewe na wana wao wala msikubali wana wenu wawaoe mabinti wao.+ 4 Kwa maana watawapotosha wana wenu waache kumfuata Mungu na kuanza kuabudu miungu mingine;+ kisha hasira ya Yehova itawaka dhidi yenu, naye atawaangamiza upesi.+

  • Yoshua 23:12, 13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 “Lakini mkimwacha na kushikamana na watu wa mataifa haya yaliyobaki+ na kuoana nao+ na kushirikiana nao, 13 mjue kwa hakika kwamba Yehova Mungu wenu hataendelea kuyafukuza* mataifa haya kwa ajili yenu.+ Yatakuwa mtego wa kuwanasa, nayo yatakuwa mjeledi wa kuwachapa mbavuni+ na miiba machoni mwenu mpaka mtakapoangamia kutoka katika nchi hii nzuri ambayo Yehova Mungu wenu amewapa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki