-
Nehemia 10:28-30Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
28 Watu wengine wote—makuhani, Walawi, walinzi wa malango, waimbaji, watumishi wa hekaluni,* kila mtu aliyejitenga na mataifa yaliyokuwa nchini ili afuate Sheria ya Mungu wa kweli,+ pamoja na wake zao, wana wao, na mabinti wao, kila mtu mwenye ujuzi na uelewaji*— 29 wakajiunga na ndugu zao, wakuu wao, wakajifunga kwa kiapo na laana, kwamba watatembea katika Sheria ya Mungu wa kweli, iliyotolewa kupitia Musa mtumishi wa Mungu wa kweli, na kufuata kwa makini amri zote za Yehova Bwana wetu, hukumu zake, na masharti yake. 30 Hatutakubali mabinti wetu waolewe na watu wa mataifa yaliyo nchini, wala hatutakubali wana wetu wawaoe mabinti wao.+
-